Sera ya Faragha

Jinsi Tunavyolinda Taarifa Zako

Kwa mujibu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya Mwaka 2022

Ilisasishwa: Januari 2026

Faragha yako ni kipaumbele chetu. Sera hii inaeleza jinsi tunavyokusanya, kutumia, na kulinda taarifa zako.

1. Taarifa Tunazokusanya

Taarifa za Msingi

Jina, namba ya simu, na barua pepe wakati wa kujisajili.

Uthibitisho

Namba ya NIDA au Picha ya Kitambulisho kwa ajili ya kupata "Blue Tick" (Hizi huhifadhiwa kwa njia ya siri ya hali ya juu).

Miamala

Kumbukumbu za michango na malipo ya matangazo.

2. Matumizi ya Taarifa

Tunatumia taarifa zako kwa ajili ya:

  • Kuthibitisha utambulisho wako ili kuzuia akaunti feki (Fake Profiles).
  • Kuchakata michango na malipo kupitia washirika wetu wa malipo.
  • Kuboresha usalama wa jukwaa na kuzuia uhalifu wa mtandao.

3. Kushiriki Taarifa na Watu Wengine

🛡️ Hatuuzi taarifa zako kwa makampuni ya biashara.

Tunaweza kushiriki taarifa zako tu:

  • Na watoa huduma za kifedha (kama Mitandao ya Simu) ili kukamilisha miamala yako.

4. Haki Zako

Chini ya Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, una haki ya:

Kuomba nakala

ya taarifa zako tunazohifadhi

Kuomba kufutwa

kwa akaunti yako na taarifa zake (Right to be Forgotten)

Kurekebisha taarifa

zisizo sahihi kuhusu wewe

Kwa maombi yoyote kuhusu taarifa zako:

Wasiliana na Timu ya Faragha →